Numbers 32:1-5

Makabila Ng’ambo Ya Yordani

(Kumbukumbu 3:12-22)

1 aKabila la Wareubeni na Wagadi, waliokuwa na makundi makubwa ya ng’ombe, kondoo na mbuzi, waliona kuwa nchi ya Yazeri na nchi ya Gileadi ni nzuri kwa mifugo. 2 bHivyo walimjia Musa, na kuhani Eleazari na viongozi wa jumuiya, na kuwaambia, 3 c“Atarothi, Diboni, Yazeri, Nimra, Heshboni, Eleale, Sebamu, Nebo na Beoni, 4 dnchi ambayo Bwana ameishinda mbele ya wana wa Israeli, inafaa kwa mifugo, nao watumishi wako wana mifugo. 5 eKama tumepata kibali mbele ya macho yako, nchi hii na ipewe watumishi wako kama milki yetu. Usitufanye tuvuke Yordani.”

Copyright information for SwhKC